Maswali 6 ya kujiuliza kabla hujaanzisha blog


maswali 6 ya kujiuliza kabla hujaanzisha blog“Je! unahitaji kuanzisha blog, kama ndio basi zingatia yafuatayo”
Kabla hujaanzisha blog na kutumia muda wako kuishughulikia ni vyema ukajitathimin mwenyewe katika mambo 6 yafuatayo;

Je! unapendelea kutumia muda wako mwingi katika mtandao wa intanet?
Kuanzisha blog, kuipromoti, na kuikuza ni kitu kinachohitaji mtu mwenye mapenzi ya kukaa katika komputa muda mwingi na kujisikia raha kwa huko kukaa kwake. Mwenye blog anahitaji muda kuandika post za blog yake, kupitia na kusoma blog za wenzake, kupitia post zake za nyuma na kuzihariri na kutafuta zana zitakazomsaidia kuifanya blog yake iwe bora zaidi. Hivyo basi kama huwa unajisikia tabu kukaa mbele ya kompyuta muda mwingi basi ni vyema ukatafuta ufumbuzi kabla ya kuanzisha blog.

Je! Unapenda kuandika?
Kuwa na blog maana yake kuwa muandishi zaidi. Hata kama blog yako itahusisha picha bado itahitaji utoe maelezo juu ya hizo picha, kujibu koment/michango ya wateja wako, kuchangia katika blog za wengine na kadhalika. Haya yote ni muhimu kwa mafanikio ya blog yako na ili yatimie basi unahitajika uwe ni mwenye kupenda kuandika-andika tena mambo yenye maana.

Je! unaguswa na kuvutiwa na mada unayoiandikia?
Ili blog yako iwe na mafanikio unahitajika uwe post mara kwa mara post zenye maana na zenye kuongeza kutu fulani kwa wasomaji wako. Hii itasaidia kufanya upate wateja wapya na uweze kuwafanya wateja wako kuwa na hamu na mahitaji ya kurudi tena katika blog yako. Ikiwa we mwenyewe hauguswi sana na mada unayoiandikia basi hautaweza kuingia katika blog yako kila siku na kuweka post mpya, ama unaweza kuweka post lakini si nzito katika uwanda unaouandikia.

Je! Una msimamo?
Kama kweli unataka kuwa mwanablog basi ni lazima uwe na msimamo na unachokifanya. Blog inataka uwe na ratiba ya kuishughulikia kila siku. Inategemea na mada uliyochagua, utahitajika uende sehemu mbali mbali kutafuta taarifa na habari zinazohusiana na blog yako, utahitajika usome vitabu na mengineyo. Yote haya yatatumia muda wako mwingi lakini ni muhimu sana ili blog yako iweze kuwa na post zenye kuwashawishi wateja wako kutembelea tena.

Je! Upo tayari na huuna hofu ya kutoa mawazo yako na fikra zako kwa jamii?
Hebu fikiria hili, limetokea jambo katika jamii na wengi wa waandishi, wanasiasa na wadau wengine katika uwanda wa jambo hilo wanasimamia upande mmoja ambao wewe unaamini mtazamo huo si sahihi. Je unaweza kuthubutu kutoa mawazo yako na kuonyesha upande unaosimamia pasi na hofu ya namna jamii itakavyo kuchukulia? Mwanablog ni mwana mapinduzi na hapaswi kuwa na uoga wa kutoa mawazo yake ambayo kwa upeo na uchanganuzi wake anayaona yanamanufaa katika kuijenga jamii.

Je! Unaogopa kuwa haufahamu mengi kuhusu teknolojia ya mtandao na haupo tayari kujifunza?
Mwanablog mwenye mafanikio hana hofu ya kuwa hajui jambo fulani katika mitandao ya intanet. Anapogundua kuwa kuna kitu kipya katika mtandao ambacho ni muhimu katika kuijenga na kuikuza blog yake basi hukitafuta, hujifunza na kukifanyia kazi. Kuna vitu vingi vya kuvifahamu kama vile HTML, SEO, CSS na mengineyo. Hata hivyo hayo si katika mambo ya msingi yanayohitajika kukufanya ufanikiwe.
Share this article :

Post a Comment

Tupende katika Facebook

 
Msaada : All Tanzania Blogs Hakimiliki © 2013. All Tanzania Blogs
Blog Imebuniwa na Kuchapwa na: Tanzania Website Design Imewezeshwa na: Blogger