Blog ni nini?

Maana ya blog:

blog ni tovuti yenye maingizo yanayoitwa machapisho (posts) ambayo huonekana  katika kwa utaratibu wa kutangulia chapisho jipya kwanza na kufuatiwa na machapisho ya nyuma. Kwa mfano kama juzi, jana na leo umeandika machapisho na kuyachapa katika blog yako basi katika kurasa yako ya mbele litaonekana kwanza chapisho la leo kisha la jana na kisha la juzi. Blog huhusisha makala unazochapa (machapisho), viungo (links) na maoni  (comments) ya watembeleaji ili kuongeza maingiliano ya kimawasiliano kati ya blog na watembeleaji blog hiyo. Kwa kawaida blog huumbwa kwa programu maalum za kuchapishia.

Program za kublog:

ü  Blogger (www.blogspot.com)
ü  Wordpress (www.wordpress.com)
ü  Drupal
ü  Movable Type
ü  TypePad
ü  Livejournal
ü  b2evolution

Mnyambuliko wa neno blog:

ü  Kublog: kitendo cha kuandaa machapisho na kuyachapa katika blog
ü  Mwanablog: mtu ambaye anaandika machapisho katika blog
ü  Ulimwengu wa blogu: jumuiya/jamii/ ya wanablog na vinavyohusiana na blog katika mtandao

Hali ya mtandao kabla ya kuanza kwa blog:

Kuanzia mwaka 1989 ulipogunduliwa mtandao (Web 1.0) hadi 2004 mtandao ulikuwa ni kama chombo cha kutolea habari tu. Wenye tovuti walikuwa wakitoa habari walizonazo lakini hapakuwa na nafasi ya kumuwezesha mtembeleaji kuweza kutoa mchango wake katika habari hizo ama kushiriki kwa namna yeyote zaidi ya kusoma na kutazama tu. Hivyo tunaita kuwa mtandao ulikuwa ni wa mazungumzo ya upande mmoja tu na kuacha upande wa pili kuwa wasikilizaji.

Baadae katika maendeleo ya mtandao kulianza kuwa na maingiliano ambapo ulianzishwa utaratibu wa kuweza kununua kupitia katika mtandao lakini bado mtandao ulibaki kuwa ni wa upande mmoja kutoa taarifa na mwingine kusikiliza.

Mwaka 2004 wakati wa mageuzi “rasmi” ya mtandao kutoka “Web 1.0” kuingia “Web 2.0” (mtandao wa kijamii) yalifanya maudhui (contents) ya mtembeleaji kuwa ni sehemu muhimu ya ulimwengu wa mtandao. Leo hii tuna mtandao ambao unajumuisha mazungumzo ya pande mbili ambapo mtembeleaji anaweza kushiriki kwa kuingiza mchango wake kwa mtindo wa maoni na njia nyinginezo za mitandao ya kijamii. Hapa ndipo blog ilipozaliwa katika ukamilifu wake tulionao sasa (Ikumbukwe kuwa blog ilikuwepo tangu miaka ya 1990 lakini hapakuwa na maingiliano na mtembeleaji)

Kuzaliwa kwa Blog:

Awali blog ilianza miaka ya 1990 kama shajara (Diary) ya mtandaoni. Watu binafsi walikuwa wakichapisha habari na matukio yao ya maisha ya kila siku na kutoa mitazamo yao juu ya mambo tofauti wanayokutana nayo katika maisha. Machapisho yalikuwa yakijipanga katika blog kwa kuanza na yale ya karibuni zaidi kisha kufuata na yaliyopita ili kuleta maana zaidi kwa msomaji.

Kutokana na maendeleo ya mtandao viliongezwa vitu vinavyowezesha kuwepo na mazungumzo ya pande mbili na kumfanya mtembeleaji kuweza kutoa maoni yake ama kuongeza kiuno katika blog ama tovuti nyingine kwenda katika blog aliyosoma ili kuongeza mjadala zaidi katika mtandao

Hali ya blog kwa sasa:

Mtandao uimekuwa zaidi wa kijamii, blogs zimepata umaarufu mkubwa katika mtandao. Leo, kuna blog zaidi ya milioni 100 na kila siku blog mpya zinaingia katika ulimwengu wa blog kila siku. Blog zimekuwa ni zaidi ya shajara za mtandaoni. Kwa kweli, wanablog wamekuwa sehemu muhimu ya ulimwengu wa mtandaoni na nje ya mtandao na wanablog maarufu wamekuwa wakileta athari kubwa katika ulimwengu wa siasa, biashara na jamii kwa ujumla.

Mustakabali wa blog:

Ni suala lisilopingika kuwa wanablog wanaonekana kuwa na nguvu zaidi katika siku zijazo na jamii na wafanya biashara wametambua uwezo wao wa ushawishi katika kuvutia masoko na kubadili muelekeo wa jambo katika jamii.

Kwa sasa kila mtu anaweza kuanzisha blog bure kabisa ilimradi uweze kupata mtandao. Swali langu kwako ni je, unayo blog kwa sasa? Kama unayo basi iweke katika kipengele cha maoni hapo chini. Kama hauna basi tuambie kwa nini huoni umuhimu wa kuwa na blog yako.
Share this article :

+ maoni + 3 maoni

9 July 2013 at 15:09

Natamani kuwe na Kiswahili cha blog. Napendekeza iitwe Kiingia Mtandaoni. Hapo tutapata kuwa kublog ni Kuingia Mtandaoni. Waonaje?

9 October 2014 at 03:22

Ni vyema kuona blog za kiswahili zikishamiri, Kwa sasa Hali ya blog ni ya kuridhisha sana hapa Tanzania.
Topic Nzuri,
Hata mimi nimecover topic kama hii kupitia.
http://chapisha.com/blog-ni-nini/

15 April 2015 at 08:23

Asante kwa kutuelimisha

Post a Comment

Tupende katika Facebook

 
Msaada : All Tanzania Blogs Hakimiliki © 2013. All Tanzania Blogs
Blog Imebuniwa na Kuchapwa na: Tanzania Website Design Imewezeshwa na: Blogger